‘Kabla hujanunua ardhi, Ni vyema kujiridhisha inaangukia katika kundi gani la umiliki’
By TP. Alpha Mangula
Umakini katika kuuza na kununua ardhi nchini Tanzania imekuwa ni zoezi ambalo linaonekana kuwa rahisi tofauti na vile inavyotakiwa kwa matakwa ya kisheria. Mara nyingi wananchi wamekuwa wakiuziana ardhi na huwatumia viongozi wa mitaa kama mashahidi wa mauziano hayo. Kutokana na kukua kwa miji na ongezeko la watu, Maeneo mengi yamekubwa na changamoto ya kuuzwa mara kadhaa au wananchi kuuziwa maeneo ambayo yametengwa kwa matumizi maalumu tofauti na makazi au hayafai kabisa kumilikiwa na mwananchi.
Tanzania, Ardhi imegawanywa katika makundi Matatu; Ardhi Kijiji (Village land), Ardhi ya Jumla (General Land), Ardhi ya Hifadhi (Reserved Land). Tujadili aida moja kwenda nyungine
ARDHI YA KIJIJI hii ni ardhi ambayo ipo chini ya kijiji, Ardhi hii mamlaka yake yamekasimishwa katika halmashauri ya kijiji (Village Council); Kwa Mujibu wa sheria, Halmashauri ya Kijiji ina jukumu la kusimamia na kuratibu matumizi ya kila kipande cha ardhi kilichopo ndani ya mipaka ya kijiji. Sheria inazitaka halmashauri za kijiji kushirikiana na Halmashauri za Wilaya Kuandaa Mipango Bora ya Matumizi ya Ardhi na kila mmliki wa ardhi ya kijiji kuwa na nyaraka ya umiliki wa ardhi ambayo huitwa Hati Miliki ya Kimila (Customary Right of Occupance – CCRO ).
Ili kuandaa Matumizi Bora ya Ardhi, Ni lazima kijiji kiwe kimepata cheti cha kijiji ambacho hutolewa na kamishna wa Ardhi baada ya kuhakikisha mipaka ya Kijiji imepimwa na ramani za upimaji wa kijiji umeidhinishwa. Lengo la kuandaa matumizi bora ya ardhi ni kutenga matumizi yanayoendana kuwa mahali pamoja ni hii husaidia kuepusha migogoro isiyo kuwa ya lazima.
ARDHI YA JUMLA hii ni ardhi iliyopo maeneo ya Mijini, Ardhi hii husimamiwa na Mamlaka za Upangaji kama vile halmashauri za wilaya, Miji, Manispaa na Majiji. Kwa kawaida maeneo haya hutangazwa kama maeneo ya mpango ‘ Decralation of Planning Area’ kwa maana hiyo kutokana na kukuwa kwa miji wakati mwingine maeneo ya vijiji huchukuliwa na kutangazwa kuwa maeneo ya mjini.
Maeneo ya Mpango Huandaliwa Mipango Kabambe ‘Master Plan’ na kufuatia mipango ya kina ‘detailed planning schemes’ na hatimaye hupimwa kabla mwananchi hajapewa nyaraka ya kumiliki ardhi ambayo huitwa Hati Miliki ya Kiwanja (Certificate of Occupancy); Kila kiwanja humilikiwa kwa kutegemea matumizi yaliyopangwa (Makala zinazofuata zitaeleza kwa kina aina za umili wa ardhi)
ARDHI YA HIFADHI hii ni ardhi ambayo inamalikiwa na mamlaka maaulumu za uhifadhi, Mfano TANAPA, TAWA, Uhifadhi wa Mabonde ya Mito, Mamlaka za Misitu na nyinginezo. Ardhi hizi huwa haziruhusiwi kutumika kwa matumizi ya makazi, kwa maana hiyo ukinunua eneo la hifadhi ya mikumi ni sawa na kupoteza fedha na aliye kuuzia anakuwa na hatia
Watu wengi wamedhulumika kwa kuto kuzingatia mambo haya madogo lakini yana tija
Kwa leo tuishie hapa, Kama una swali au maoni au ungependa tuzungumizie kitu gani usisite kutuandikia na tutatlifanyia kazi, Asante







